Jumatatu, 20 Machi 2017

YAJUWE MAMBO YA KUMFANYIA MTU ANAPOKARIBIA KUFA NA NINI KIFANYIKE PUNDE ATAKAPOKUFA?


Mambo muhimu anayofanyiwa Muislamu (mtu) anayekaribia kufa.
Mtu akikaribia kufa huwa hajiwezi kwa lolote lile pamoja na elimu, ujuzi alionao, hivyo huhitajia kufanyiwa mambo yafuatayo;
                         i.            Kuogeshwa, kugishwa mswaki na kumpaka mafuta au manukato kama kuna uwezekano.
                          ii.            Kumlaza kwa ubavu wa kulia au chali na kumuelekeza Qibla iwapo kuna uwezekano.
                          iii.            Kumpa maji ya kunywa.
                          iv.            Kutamka (kumsomea) –  Shahada “Laa ilaha illallaah”
Abu Said na Abu Hurarirah wamesimulia kuwa, Mtume wa Allah amesema: “Wasomeeni watu wenu wanaokaribia kufa; ‘Laailahaillallaah”

Pia Mu’az bin Jabal amesema kuwa Mtume (s.a.w) amesema: “Yule ambaye maneno yake ya mwisho yatakuwa; “Laailahaillallaah” ataingia peponi.
                        (Abu Daud) 
            -  Si lazima anayekufa aitamke kwa sauti, inaweza ikawa kimoyo moyo.

Mambo anayofanyiwa mtu (maiti) mara tu baada ya kufa.
Baada ya mtu kufa inatuwajibikia tuseme: “Innalillah wainnailaihraaji’una”. Qur’an (2:156). Kisha kumfanyia maiti mambo yafuatayo:

                                            i.            Kwa taratibu kurudishia mdomo wake usiwe wazi kwa kufunga kwa    kitambaa kutoka kidevuni na kuzungushia kichwani.

                                          ii.            Kufunga macho ya marehemu na huku ukisema;
Kwa jina la Allah na kwa kufuata mila ya Mjumbe wa Allah, Ewe Mola wetu mrahisishie mambo yake ya sasa na msahilishie mambo yake ya baadaye. Na jaalia anayokutanayo yawe bora kuliko aliyoyaacha.”

                                        iii.            Lainisha viungo vyake (miguu na mikono) kwa kukunja na kukunjua taratibu.
       -    Kama kuna ugumu maji ya uvuguvugu au mafuta yanaweza kutumika    kulaisha na kunyoosha viungo hivyo.
      -     Baada ya kulainisha viungo, miguu na mikono inyooshwe na kulazwa uso   ukielekezwa Qibla kwenye mkeka au kitanda kisicho na godoro. 

                                        iv.            Maiti avuliwe nguo zote alizokufa nazo na kisha kufunikwa kwa shuka kubwa
-     Ni vyema afunwe kitambaa tumboni au kuwekewa kitu kizito ili tumbo lisifutuke.

                                          v.            Marashi na ubani vitumike kwa wingi ili kuzima harufu ya uvundo wa maiti.