Jumamosi, 6 Mei 2017

KUAMINI QADAR YA ALLAH


Kuamini Qadar ya Allah (s.w)

o Maana ya Qadar
Kilugha: maana yake ni kipimo, kiasi au makadirio.
Rejea Qur’an (54:49), (25:2), (36:39).
Kisheria: ni mpango (plan) wa Allah (s.w) unaohusu kutokea, kuwepo na hatima ya maumbile na viumbe vyake vyote na matukio yatakayopelekea kutokea na kuondoka kwake.
Rejea Qur’an (57:22), (6:59)

o Maana ya Qudra

Ni uwezo wa Allah (s.w) usio na mipaka katika kufanya chochote na lolote atakavyo kwa kuliambia “kuwa” na linakuwa.

o Umuhimu wa Kuamini Qadar ya Allah (s.w)

(i) Kuamini Qadar ya Allah (s.w) ni nguzo ya sita katika nguzo za imani ya Kiislamu.

(ii) Kuamini Qadar ya Allah (s.w) kikweli kweli ndio msingi wa imani sahihi ya muumini juu ya mipango na uwezo wa Allah (s.w).

(iii) Kutoamini Qadar ya Allah (s.w) ni miongoni mwa makosa yatayoharibu itikadi ya mja juu ya utendaji na mwenendo wake.

(iv) Hakuna chochote kitakachofanyika au kutokea kwa viumbe isipokuwa kimeandaliwa na kupangwa na Allah (s.w).


o Mtazamo wa Uislamu juu ya Qadar

a) Ni makosa makubwa kudhani kuwa mtu anaweza kufanya jambo lolote lile kinyume na Qadar ya Allah (s.w).


b) Ni makosa makubwa mtu kumlaumu Allah (s.w) kwa maovu anayoyatenda kuwa ndiye amemkadiria kuyafanya.
Uk. 23 kati ya 1 3 1


c) Allah (s.w) anayajua yote atakayoyafanya mja hadi hatima ya maisha yake siku ya Qiyama hata kabla ya mtu huyo hajazaliwa.

Rejea Qur’an (11:6)

d) Isidhaniwe kuwa maadamu mtu amechagua kumuasi Allah (s.w) basi Allah (s.w) hana uwezo wa kumzuia, bali atafanya hivyo tu iwapo lipo katika Qadar ya Allah.


e) Utatanishi wa Qadar huondoka kwa kuzingatia maeneo makuu mawili;

i. Eneo la hiari (uhuru) ambalo mtu huchagua kufanya jambo jema au baya atakalo.

ii. Eneo lisilo la hiari kwa mtu kuamua kufanya jambo lolote atakalo, mfano; kuchagua wazazi wa kumzaa, sehemu, muda wa kuzaliwa, jinsia, n.k.


f) Mtu ataulizwa au ataadhibiwa kwa matendo ya hiari tu ambayo ana uhuru nayo wa kuchagua lipi afanye na lipi asifanye.


g) Mwanaadamu hataulizwa kamwe matendo yasiyokuwa hiari kwake, mfano; kwa nini aliumbwa mweusi, mrefu, wa kike, wa kiume, kabila au nchi fulani, n.k.


o Kueleweka vibaya kwa Qadar na Qudra ya Allah (s.w)

Baadhi ya Waislamu na watu wengine wanapotosha maana na nafasi ya Qadar na Qudra ya Allah (s.w) kama ifuatavyo;

i. Kuacha kutekeleza wajibu wao kwa Allah kwa kusingizia kuwa “imeshaandikwa kwenye kitabu cha Allah kuwa sisi hatutatekeleza au tutatekeleza jambo fulani”


ii. Baadhi ya watu wanaojiita waislamu kuacha kutekeleza amri za Allah (s.w) kama swala, funga, n.k. kwa kusingizia kuwa hawajajaaliwa kufanya hivyo na watatekeleza pindi watakapojaaliwa.


iii. Baadhi ya watu, miongoni mwa waislamu hufanya maovu kwa shangwe kwa kudai kuwa hivyo ndivyo alivyokadiriwa na Allah (s.w) na wasingeweza kukwepa Qadar yake.
Uk. 24 kati ya 1 3 1


iv. Baadhi ya watu kudai kuwa, “Allah (s.w) mwenyewe ameshajua na ameshapanga kuwa watu wa motoni au peponi, hivyo hakuna haja ya wao kufanya uovu au wema”.


v. Watu wengine wanadai kuwa, “Allah (s.w) amewapendelea wengine kwa kuwapangia kwenda peponi huku akiwadhulumu wengine kwa kuwapangia kwenda motoni.

Madai haya hutiliwa nguvu hata kwa ushahidi wa aya za Qur’an kama ifuatavyo;

Rejea Qur’an (39:36-37), (29:62), (2:284), n.k