Alhamisi, 21 Septemba 2017

SABABU ZA UGONJWA WA KISUKARI

SABABU ZA UGONJWA WA KISUKARI
Ugonjwa wa kisukari ni ugonjwa unaotokea pale ambapo mwili unaposhindwa kuzalisha homon za insulin au mwili kushindwa kuzalisha homon za insulin za kutosha au mwili kushindwa kutumia homon za insulin. Wakati mwingine hutokea pale mfumo wa  kinga mwilini (immune system) unapoathiri organ ya pancrease na kuathiri uzalishaji wa homon ya insulin.

Ugonjwa wa kisukari husababishwa na mabo mengi yakiwepo kurithi kutoka kwenye familia, mazingira na ufumo mbaya wa maisha (life style). Japkuwa ugonjwa wa kisukari huweza kurithi kutoka kwa wazazi au familia lakini mfumo mbaya wa maisha huchangia kwa kiasi kikubwa pia katika kusababisha ugojwa huu wa kisukari. Katika post hii nitazungumzia kwa namna gani mfumo mbaya wa maisha unavyoathiri kupatikana ugonjwa wakisukari.
  1. Kuzidi uzito mwilini; kikawaida mwili unahitaji uzito maalumu kulingana na kanuni za afya. Uzito ukiwa mkubwa sna ni tatizo na ukiwa ni mdogo sana pia ni tatizo. Uzito kuwa mkubwa zaidi unapelekea homon ya insulin kutokuzalishwa kiwango kinacho takiwa au mwili kushindwa kutumia insulin vizuri (insulin resistance). Zipo njia nyingi za kupunguza uzito zikiwepo kupitia vyakula, mazoezi au kubadilisha mfumo wa maisha. Hakikisha kuwa uzito wako upo katika hali ya kawaida. Muone daktari akupe ushauzi kuhusu uzito wako.


  1. Kutokufanya mazoezi; kikawaida mazoezi yana faida kubwa sana mwilini, zikiwemo kuufanya mwili uwe imara. Mazoezi huweza kusaidia mifumo mbalimbali ya mwili kufanya kazi vizuri kama vile mfumo wa chakula, mfumo wa damu na mfumo wa afya. Mazoezi huweza kumkinga mtu na magonjwa ,mbalimbali kama vile mafua, presha ya damu, shambulio la moyo na kisukari. Mazoezi hupunguza mlundikano wa mafuta kwenye mwili na kusaidia kuondowa uchafu mwilini kwa njia ya jasho. Kiafya inashauriwa mtu afanye mazoezi japo kwa wiki asikose mara tatu. Yapo mazoezi mengi tuu na yasiyo na haja na kujiumiza saana kama vile kuruka kamba au kukumbia jogging.


  1. Mpangilio wa lishe, chakula ni muhimu kwa maisha ya kiumbe chochote, ila ulaji mbaya pia ni tatizo kwa afya ya kiumbe pia. Mtu anatakiwa ale chakula kwa namna ambayo haitamletea madhara katika afya yake. Mtu anatakiwa ale chakula ambacho hakitamletea kuzidi uzito au utapia mlo au kitambi. Haya huenda yakawa na madhara katika afya ya mtu na hatimaye kupata kisukari. Chakula chenye mafuta mengi, sukari nyingi ama chumvi nyingi vyote sio vizuri kutumia.

  1.  Mazingira; wakati mwingine inatokea mazingira watubwanayoishi yakapelekea kupata kisukari kwa mfano  mashambulizi ya virusi. Kuna aina ya virus ambao wanashambulia mwili na kufanya mwili kushindwa kusazalisha homoni za kutosha kwa ajili ya kushibiti kiwango cha sukari ndani ya damu.
  2. Kutithi; unaweza kupata ugonjwa wa kisukari kwa njia ya kurithi kutoka katika familia. Kama ilivyo kwa magonjwa mengine ya kurithiwa kwa kupitia vizazi au kurithi rangi ya ngozi urefu au ufupi kutoka kwa wazazi vivyo hivyo kisukari huweza kurithiwa. Haijalishi kati ya baba nani ana kisukari lakini huenda ukakipata kwa kurithi. Pia huenda wazazi wakakwa na kisukari na wewe ukakisosa pia.

Hitimisho
Ijapokuwa ugonjwa wa kisukari ni hatari sana lakini kama mtu atafata masharti anaweza kuishi maisha mazuri tuu kama watu wengine. Jambo la msingi hapa ni kufuata masharti na kuendelea kutumia dawa za kisukari . Kufanya mazoezi na kubadilisha utaratibu wa chakula.