Alhamisi, 19 Oktoba 2017

ZIJUWE DALILI ZA UGONJWA WA SARATANI

  DALILI ZA UGONJWA WA SARATANI

Ugonjwa wa saratani hutokea pale seli za mwili zinapokuwa bila ya mpangilio maalumu na kusababisha uvimbe. Uvimbe huu huenda ukawa mkubwa zaidi na kusababisha uharibifu wa viungo vya mwili kama maini ubongo na mishfupa. Uvimbe huu pia hueza kusambaa mwilini na kusababisha vimbe mbalimbali ndani ya mwili.

Kikawaida seli ndani ya mwili huzaliwa na baadaye huweza kufa baada ya kipindi maalumu. Kwa mtu mwenye saratani seli hizi hazifi hivyo huendelea kukuwa bila ya mpangilio. Seli hizi huweza kuingia kwenye mfumo wa damu na kusambazwa kuelekea sehemu zingine za mwili na hatimaye kusambaa kwa saratani viungo vingine vya mwili.


Katika sababu za kutokea kwa saratani ni pamoja navyakula 35%, sigara30%, mionzi ya jua 10%, virus 7%, shughuli za kazi 4%, pombe 3%, mionzi 1% na sababu nyinginezo kwa 10%. Hivyo hapa utaona kuwa vyakula na uvutaji wa sigara vipo katika msitari wa mbele kusababisha ugonjwa wa saratani.

Mwaka 200 WHO wametowa ripooti inayoeleza kuwa ugonjwa wa saratani ndio unaoongoza kwa kusababisha vifo vya watu wengi duniani.mwaka 2004 watu milioni 7.4 wamefariki kwa ugonjwa wa saratani ambayo ni sawa nsa 13% ya vifo vyote vilivyotokea duniani mwaka huu. Saratani ya maini, tumbo, utumbu na saratani ya matiti ndo zimeongoza kwa vifo vya watu duniani. Vifo vinavyosababishwa na saratani vinatarajiwa kuongezeka kila siku na vinatarajiwa kufikia milioni 12 ifikapo mwaka 2030. (WHO. 2009).

Dalili za ugonjwa wa saratani hutofautiona sana kulingana na aina ya saratani ambayo mtu anayo. Zipo aina zingine za saratani hazioneshi dalili zozote mpaka zitakapokuwa zimeenea vizuri mwilini. Ingawa hali ipo kama hivyo lakini wataalamu wa afya wameonesha baadhi ya dalili ambazo zinaonekana kwa watu wengi wanaopata saratani ambazo ni;-

1. Homa;
Haya ni maumivu ya kishwa yasiojulikana chanzo chake. Maumivu haya sio ya ugonjwa wowote wenye kuonekana, hata mgonjwa akipimwa huenda asikutwe na kitu chochote .maumivu haya ni yenye kuendelea kwa muda mrefu

2. Uchovu;
Huu ni uchovu ambao hauishi katu. Hata mtu apate muda wa kupumzika lakini katu uchovu huu hautaondoka. Japo mgonjwa wa kisukari pia hupata uchovu kama huu lakini saratani ina uchovu wa kipekee. Hivuyo ni vizuri kumuona daktari akwambie aina ya uchovu ulonao.
3. Mabadiliko katika mfumo wa chakula;
Mabadiliko haya ni pamoja na kushindwa kumeza chakula au kukosa choo. Dalili hizi huenda zikafanana na magonjwa mengine, hivyo ukiona mabadiliko haya wahi ukamuone daktari.

4. Kushindwa kupumua vizuri;
Saratani ya mapafu huweza kuonesha dalili hii ya kushindwa kupumuwa vizuri. Hii hutokea pale ambapo kuna vimbe sa saratani katika mfumo wa upumuaji. Inaweza kuwa kwenye mapafu au koo.

5. Kikohozi;
Hiki ni kikohozi ambacho sababu yake hasa ni ngumu kujulikana. Kikohozi hizi hakisikii dawa yoyote na ni chenye kuendelea. Saratani katika mfumo wa upumuaji kama mapafu huweza kuonesha dalili hii

6. Mabadiliko katika ngozi;
Hapa ngozi inaanza kubadilika rangi. Pia vimbe ndani ya ngozi huanza kutokea. Madoa meupe kwenye ngozi, mdomo, na kwenye ulimi. Pia mtu anaweza kuwa na makovu ambayo hayaponi.

7. kutokwa na damu;
Damu zinaweza kutoka katika maeneo mbalimbali kama vile sehemu ya haja kubwa na haja ndogo kwa wanaume na wanawake. Pia damu huweza kutoka kwenye matiti ambayo ni dalili ya saratani ya matiti.

8. Uvimbe kwenye matiti na korodani;
Huu ni uvimbe usio wa kawaida ambao unaanza kukuwa kwnye matiti kama dalili ya saratani ya matiti. Wakati mwingine ngozi ya matiti inakuwa ngumu. Hali hii pia hutokea kwenye korodani ambapo kunatokea uvimbe usio wa kawaida. Vimbe hizi pia huweza kusababishwa na mambo mengine hivyo hakikisha unamuona daktari kwa mabadiliko haya.

9. Kupoteza fahamu au kifafa;
Kwa saratani ya ubongo huweza ikamfanya mtu aweze kupoteza fahamu. Pia hutokea mtu akaanza kupata aina za kifafa. Saratani hii hutokea pale ubongo uapotengeneza uvimbe.

Hitimisho;

Ushauri wangu ni kuwa watu waishi kwa uangalifu kwani matibabu ya saratani ni ya gharama kubwa sana ni ni machache hutolewa bure. Halikadhalika hospitali zinazotowa matibabu ya saratani ni chache pia.