Alhamisi, 7 Juni 2018

IJUE ZAKAT AL-FITR NA LAYLAT AL-QADIR



USIKU WA LAYLAT AL-QADIR.
Asalaamu 'alaykum
Sifanjema zinastahiki kusifiwa Allah Mola wa ulimwengu. Salana Salamu zimuendee kipenzi cha umma huu Mtume Muhammah (s.a.w). huu ni mwendelezo wa Darsa za Funga ambapo tutajifunza Kuhusu usiku huu wa Laylat al-qadir pamoja na Zakat al-fitr. Tunamuomba Allah atupe Afya na uzima katika kulitekeleza hili. Pia unaweza kuzipata Darsa hizi bila ya kuhitajia intanet ukiwa na program yetu ya simu (Android App). unaweza kuidaunload kwa kubofya hapa. Unaweza pia kusoma darsa nyenginezo kwa kubofya link zifuatazo;-
1.Darsa za funga bofya hapa
2.Darsa za Dua bofya hapa
3.Mafunzo ya tajwid (kusoma quran) bofya hapa
4.Quran Juzuu 'Amma bofya hapa



FADHILA ZA USIKU HUU
Allah ameiteremsha Quran kwenye usuku huu. Allah amesema “hakika sisi tumeitetemsha (quran) katika usiku wa laylat al-qadir” (quran 92:1)
Allah ametukuza sana ukisu huu hata akasema kuwa ni mbora kuliko miezi elfu moja. Allah amesema “(siku wa) laylat al-qadir ni mbora kuliko miezi elfu moja (quran 97:3)

Hushuka malaika ndani ya usiku huu, na jibrili akiwemo. Pia maulamaa wamsema kuwa maana ya aya hii ni kuwa hushuka malaika na rehema, baraka na utulifu. Pia wamesema maulamaa kuwa hushuka malaika na kila amri ambayo Allah ameihukumu katika mwaka mzima huu kama alivyosema Allah katika surat dukhan aya ya 4-5.

Amani hushuka ndani ya usiku huu kuwashukia waumini mpaka alfajiri.

Amesimulia hadith Abuuhurairah kuwa mtume (s.a.w) amesema “mwenye kufunga ramadhani kwa imani na kutaraji malipo kwa Allah atasamehewa madhambi yake yalotangulia. Na mwenye kusimama katika usiku wa laylat al-qadir (akifanya ibada) kwa imani na kutaraji malipo kwa Allah atasamehewa madhambi yake yalotangulia. (Bukhari na Muslim).







        
NI UPI USIKU HUU?
Hakuna shaka juu ya kuwa usiku huu unapatikana kwenye mwezi wa ramadhani kama Alivyosema Allha kuwa ameiteremsha quran kwenye usiku huu,(quran 97:1). Na amesema pia kuwa mwezi wa ramadhani ndio mwezi ambao qurani imeteemshwa.(quran 2:185).

Na Ibn Hajar amezungumza kuwa maulamaa wametofautiana juu ya kuutambua usiku hii ni wa mwezi ngapi?, kauli zao zinafika mpaka 40. Miongoni mwa kauli hizo ni kama:-

1.maulamaa wengi wamekubaliana kuwa usiku huu unapatikana katika kumi la mwisho la mwezi wa ramadhani. Kauli hii inaegemea hadithi aloisimulia Abuu Sa’id al-khudriy kuwa Mtume (s.a.w) amesema “….utafuteni (usiku wa laylat al-qadir) katika kumi la mwisho” (Bukhari na Muslim)

2.na maulamaa wengi wamekubaliana kuwa usiku huu unapatikana katika masiku yaliyo witir kwenye kumi la mwisho yaani mwezi 21, 23, 25, 27, na 29. Maelezo haya yanaegemea kauli ya Mtume aliposema “kesheni kuutafuta usiku wa laylat al-qadir katika masiku yaliyo witiri katika kumi la mwisho” (Bukhari)

3.na kauli za maulamaa wengi wamekubaliana kuwa usiku huu ni wa mwezi 27. Na kauli hii ndiyo pia walivyokuwa wakiamini wengi katika maswahaba (Allah awaridhie wote) na kauli hii pia inaegemea hadithi sahihi kama alivyopokea Muslim na Tirmidh)

Jambo la ufupi ni kuwa usiku huu kwa hakika haujulikani kuwa ni upi ila bila shaka upo kumi la mwisho katika masiku yaliyo witir. Mtume amesema kuwa: “mimi niliuona usiku wa laylat al-qadir kisha nikasahau.….” (Bukhari na Muslim)

Usiku huu umefichwa ilikwamba tujibidiishe kumuabudu Allah sana katika kumi lote la mwisho. Mtume (s.a.w) alikuwa akikesha usiku kufanya ibada kumi la mwisho .na alikuwa aliwaamsha wakeze kufanya ibada katika kumi hili la mwisho. Usiku huu umefichwa na mtume alipoujua alitaka kuwaeleza maswahaba na akasahau. (Bukahari) soma zaidi hapa ukiwa na App yetu.

NINI MTU AFANYE KATIKA USIKU HUU?
1.kusimama kwa ajili ya ibada 

Mtume alikuwa lifikapo kumi la mwisho akijitahidi sana kufanya ibada kuliko nyakati zingine. (Buhari na Muslim). Mtume alikuwa akikaza msuli wake na kujifunga nguo kisawasawa, na alikuwa akikesha na akiwaamsha wakeze (watu wa familia yake kufanya ibada usiku) (Bukhari na Muslim)

2.kuomba dua na adhkar mbalimbali
Imesimuliwa kuwa ‘Aisha (r.a) alimuuliza Mtume amfundishe nini aseme katika usiku wa laylat al-qadir Mtume akamjibu sema “ALLAHUMMA INNAKA ‘AFFUWUN TUHIBUL-’AFWA FA’AF-’ANNI” (Tirmidh na Ibn Majah)



1.hakuna upepo unaovuma na anga lake hutulia na jua huchomoza likiwa dhaifu (halichomi)
2.Kunakuwa na utulivu
3.Wajawema wanaweza kuuona kwenye ndoto
4.Jua litachomoza asubhi likiwa safi na halichomi 
soma zaidi hapa ukiwa na App yeti

ZAKAT AL-FITR
Hii ni zaka inayotolewa kwa ajili ya fitr. Yaani huliwa sikuile ya kufungua kutoka kwenye funga ya ramadhani. Hutolewa kwa kuwatosheleza wale wenye shida ya shakula na kuingiza furaha kwa wasiojiweza siku ya ‘idi na pia ni kwa ajili ya kutakasa funga za walofunga mwezi wa ramadhani. Funga hutakaswa kwa yale yalotuponyoka na tukafanya maovu katika mwezi wa ramadhani. (Abuu Daud na Ibn Majah ). Pia zaka hii hutolewa kabla ya kutoka kwenye swala ya ‘id na mwenye kuitoa baada ya swala ya ‘id itakuwa ni sadaka kama sadaka zingine na si zaka. (Abuu Daud na Ibn Majah kwa isnad sahih).

Hukumu ya zaka hii ni faradhi kama ilivyokuja kauli kuwa Ibn ‘Umar amesema: “amefaradhisha Mtume (s.a.w) zaka ya fitir pishi la tende au ngano kwa mtumwa na kwa huru wanaume na wanawake, watoto na wakubwa katika waislamu na akaamrisha itekelezwe kabla ya kutoka kwenye swala ya ‘id (Bukhari na Muslim).



1.kila muislamu kama hadithi ya hapo juu ilivyo taja
2.Mwenye kuweza juu ya kutoa zaka hii

Zaka hii hutolewa kiasi cha kilo mbili na nusu (2.5) kwa kipimo cha juu. Wapo walosema mbili na robo. Pia hutolewa chakula ambacho hupendwa kuliwa eneo lile kwa kauli za maulamaa. Kwa mfano kwetu Tanzania ni Mchele. Pia utawapa watu wasiojiweza kama masikini. Maulamaa pia wamejuzisha kutoa pesa kwa hesabu ile ya zaka hii.