Jumatatu, 27 Machi 2017

YAJUWE MAANDALIZI YA KUMUOSHA MAITI NA UTARATIBU MZIMA WA KUMUOSHA MAITI

        Image result for grave muslim picture



       Kuoshwa kwa MAITI (Kukoshwa).
·         Mazingatio kabla ya kuosha maiti.
(a)    Maiti ya kiume ioshwe na wanaume na maiti ya kike ioshwe na wanawake pia.
-  Maiti ya mtoto yaweza kuoshwa na yeyote.
-  Ni Sunnah mke kumuosha mumewe na mume kumuosha mkewe pia

(b)   Ni mtu mmoja tu ndiye anayeosha na mwingine ni kwa ajili ya kumpa msaada inapobidi.
(c)    Ni muhimu muoshaji afahamu masharti ya kuosha maiti muislamu kama vile;
o   Muoshaji awe muislamu.
o   Mahali pakuoshea pawe faragha (pamesitirika).
o   Maiti aoshwe huku amefunikwa gubi-gubi na nguo nyepesi inayoruhusu maji kupenya kwa urahisi.
o   Ni vyema muoshaji asiishike maiti bali aoshe akiwa amevaa ‘gloves’.
o   Kuzingatia masharti ya mwenye kuoga josho la wajibu; kama vile kuwa na maji mengi na safi, pasiwe na kizuizi cha maji kupenya, n.k.

(d)   Ni muhimu muoshaji afahamu nguzo na sunnah za kuosha maiti kama ifuatavyo;
 -   Nguzo za kuosha maiti ni mbili:
o   Nia
o   Kueneza maji mwili mzima wa maiti.
                        -   Ni Sunnah kumuosha maiti mara tatu au zaidi kwa idadi ya witiri.



§  Namna ya Kuosha Maiti hatua kwa hatua.
                                                        i.            Maiti awekwe juu ya kitanda chenye tobo katikati ili kupitisha uchafu unaotoka tumboni.
                                                      ii.            Pawepo na shimo (ufuo) usawa wa tobo la kitanda, kama hakuna uwekano chombo kiwepo cha kukingia uchafu unaotoka kwa maiti.
                  -  Pia maiti inaweza kuoshewa bafuni au kwenye karo liliotengenezwa
                     kwa kazi hiyo.

                                                    iii.            Maiti afunikwe na nguo moja kubwa yenye kupenyeza maji wakati wa kuosha.

                                                    iv.            Maiti akalishwe juu ya kitanda usawa wa tobo na shimo (ufuo) na ainamishwe nyuma kidogo, kama ni mzito ni vizuri msaidizi wa muoshaji amuegemeze kwenye magoti yake.

                                                      v.            Muoshaji apitishe mkono wa kushoto kwenye tumbo la maiti na kuliminyaminya taratibu ili kutoa uchafu ndani.

                                                    vi.            Amlaze chali na kuminyaminya tumbo lake kama ilivyo mara ya kwanza.

                                                  vii.            Aikalishe tena na apitishe mkono wa kushoto chini akiwa amevaa kitambaa au gloves na kusafisha tupu mbili kwa maji safi.
-   Kama hapaja takata, basi na avae gloves safi na ile chafu aitupe kwenye 
                       ufuo na asafishe tena kama mara ya kwanza mpaka patakate.

                                                viii.            Baada ya hapo, muoshaji afunge kitambaa safi kwenye kidole chake shahada na akichovye kwenye maji na kumswakisha maiti meno yote na kisha akitupe ufuoni.

                                                    ix.            Muoshaji azungushe kitambaa kingine safi kidole chake kidogo mkono wa kushoto na kumsafisha nacho maiti tundu za pua kisha akitupe ufuoni.

                                                      x.            Asafishe kucha za maiti kwa kijiti safi na laini iwapo ni ndefu na chafu.

                                                    xi.            Kisha amkalishe maiti na amtawadhishe kwa kufuata taratibu za kawaida za kutia udhu (kutawadha).

                                                  xii.            Maiti akiwa amekalishwa, ataanza kumuoshwa kichwa akiwa ameinamishwa mbele kidogo.
- Kama nywele au ndevu ni nyingi zichanwe na kuoshwa kwa sabuni na
   maji mpaka zitakate.
                        - Mwanamke mwenye nywele nyingi zisukwe mikia, na zilizong’oka
                           ziambatanishwe na sanda.

                                                xiii.            Baada ya kuoshwa kichwa, maiti italazwa kwa ubavu wa kushoto na kuanza kuoshwa ubavu wa kulia, mbele na nyuma kwa pamoja kwa sabuni na maji safi mpaka itakate.

                                                xiv.            Kisha itaoshwa ubavu wa kushoto kama ilivyooshwa wa kulia.

                                                  xv.            Baada ya makosho (maosho) haya mawili, la maji na sabuni na la kuondoa sabuni, kosho la tatu la maji liwekewe karafuu na marashi ili kulegeza viungo (maungo) vya maiti.

                                                xvi.            Baada ya makosho matatu haya, muoshaji anyooshe viungo vya maiti na kumlaza kama alikuwa mara tu baada ya kufa.


                                              xvii.            Kisha achukue nguo kavu na kumfuta maiti, na baada ya hapo maiti awekwe juu ya mkeka mkavu na kufunikwa kwa nguo kavu tayari kuvalishwa sanda (kukafiniwa).