Ijumaa, 24 Machi 2017

ZIJUE AINA 12 ZA SWALA ZA SUNNAH

                   2 Kusimamisha Swala za Sunnah. 
§  Umuhimu wa Kusimamisha Swala za Sunnah.
a)      Kusimamisha swala za Sunnah ni kumtii na kumuiga Mtume (s.a.w).
Rejea Qur’an (33:21) na (3:31).

b)      Hutupelekea kuwa Wacha-Mungu kwa njia nyepesi kupitia utii na kujikurubisha zaidi kwa Allah (s.w).

c)      Hutupelekea kufikia lengo la swala kwa kujitakasa na mambo machafu na mavu.
Rejea Qur’an (29:45).

d)      Swala za Sunnah pia hujaziliza mapungufu ya swala za faradhi ambazo hazikuswaliwa kikamilifu kutokana na udhaifu wa kibinaadamu.


§  Aina za Swala za Sunnah.
Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 150-165.
Swala za Sunnah ni nyingi, tutaangalia baadhi tu kama ifuatavyo:

                                            i.            Swala ya Maamkizi ya Msikiti.
-     Huswaliwa rakaa mbili muda wowote mara tu muislamu aingiapo msikitini kabla ya kukaa.
                 
                                         ii.            Swala za Qabiliyyah na Ba’adiyyah.
      -     Hizi huswaliwa kabla (Qabiliyyah) na Baada (Ba’adiyyah) ya swala za Faradh.
      -     Ziko aina mbili; ‘Mu’akkadah’ (zilizokokotezwa) na ‘Ghairu Mu’akkadah’ (Hazikukokotezwa).
            Rejea Kitabu cha 1, EDK, Shule za Sekondari, Uk. 152.

                                       iii.            Swala ya Witiri.
-     Huswaliwa rakaa kwa idadi ya witiri; 1, 3, 5, 7, 9 na 11 katika theluthi ya mwisho wa usiku au mara tu baada ya swala ya Ishaa.
      -     Witiri imekokotezwa mwisho wa usiku zaidi na huambatanishwa kwa dua ya Qunuti katika rakaa ya mwisho.

                                        iv.            Swala ya Tahajjud (Qiyaamul-layl).
-     Huswaliwa rakaa 8 usiku wa manane kwa rakaa mbili mbili na kumalia 3 za witiri na kutimia rakaa 11.
-     Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu cha Qur’an.
      Rejea Qur’an (17:79), (25:64), (39:9) na (73:1-4).

                                           v.            Swala ya Tarawehe (Qiyaamu Ramadhan).

-     Ni swala ya kisimamo na Kisomo kirefu cha Qur’an, Juzuu 1 kila siku inayoswaliwa mwezi wa Ramadhani tu baada ya Ishaa au kabla ya swala ya Alfajir.
-     Kuna hitilafu kwa idadi ya rakaa, kauli zinasema ni rakaa 8, 11, 20, 36, n.k.lakini yenye nguvu ni rakaa 8 na 3 za witiri na kuwa jumla rakaa 11.

                                        vi.            Swala ya Idil-Fitr na Al-Udhuhaa.
-     Zote huswaliwa rakaa mbili, Idil-Fitr huswaliwa mwezi 1 Shawwal baada ya kumalizika funga ya mwezi wa Ramadhani.
-     Idil-Al-Udhuhaa huswaliwa mwezi 10 Dhul-Hija baada ya kukamilika ibada ya Hija kila mwaka.

                                      vii.            Swalatudh-Dhuhaa.
-     Huswaliwa kila siku baada ya Jua kupanda kiasi cha mita tatu kutoka kuchomoza kwake.
-     Huswaliwa rakaa mbili mbili hadi kutimia nane, lakini kwa uchache huswaliwa rakaa mbili.

                                   viii.            Swalatul-Istikharah.
-     Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada na mwongozo kwa Allah juu ya uamuzi au utatuzi wa jambo lolote zuri.

                                        ix.            Swala ya Kukidhi Haja.
-     Ni swala inayoswaliwa muda wowote kwa ajili ya kuomba msaada au utatuzi wa tatizo lililotokea au unalohitajia.

                                          x.            Swalatut – Tawbah.
-     Huswaliwa rakaa mbili muda wowote kwa ajili ya kutubia baada ya muislamu kufanya kosa.
      Rejea Qur’an (3:135-136).

                                        xi.            Swala ya Kupatwa kwa Jua na Mwezi.
-     Huswaliwa kwa jamaa, rakaa mbili, rukuu mbili kwa kila rakaa moja. Huswaliwa kwa kisimamo na kisomo kirefu mpaka Kupatwa kuondoke.

                                     xii.            Swala ya Kuomba (Swalatul-Istisqaa).
-     Ni swala ya rakaa mbili kwa ajili ya kuomba mvua baada ya kuzidi dhiki na ukame, kwa jamaa na uwanjani.
-     Swala hii ina khutuba mbili na takbira kama inavyoswaliwa swala za Idi.