Jumapili, 15 Oktoba 2017

JE! WAJUWA NI KWA NINI QURAN IMESHUSHWA KWA LUGHA YA KIARABU?

                Lugha ya Qur-an:
Lugha iliyotumika katika Qur-an ni Kiarabu sanifu kama tunavyojifu nza katika Qur-an yenyewe:

"Na namna hii tumekufunulia Qur-an kwa Kiarabu iii uwaonye watu wa Makka na walio pembezoni mwake. Na uwaonye siku ya mkutano, siku isiyo na shaka. Kundi moja litakuwa Peponi na kundi jingine Motoni          "(42:7)

              Kwa nini Qur-an Imeshushwa kwa Lugha ya Kiarabu?
Walimwengu walio wengi wakiwemo baadhi ya Waislamu wanaitakidi kuwa lugha ya Kiislamu ni Kiarabu na Uislamu ni dini ya Waarabu. Bila shaka mawazo haya yamejitokeza kutokana na kutoujua Uislamu kwa upeo wake. Uislamu ni Dini ya Walimwengu wote wa nyakati zote na ni Dini iliyofundishwa na Mitume wote. Je, Mitume wote walikuwa Waarabu au watu wote waliolinganiwa na Mitume hao na kuwafuata walikuwa Waarabu? Bila shaka jibu litakuwa "hapana". Bali tunajifunza katika Qur-an yenyewe kuwa Allah (s.w) amewajaalia walimwengu kuzungumza lugha mbali mbali na ni katika ishara ya Uungu wake na utukufu wake.

"Na katika Ishara zake (zinazoonyesha uwezo wake) ni kuumba mbingu na ardhi, na kuhitilafiana lugha zetu na rangi zenu. Kwa yakini katika haya zimo ishara kwa wenye ujuzi." (3 0:22)

Kwa nini Qur-an imeshushwa kwa lugha ya Kiarabu? Jibu lake linapatikana ndani ya Qur-an yenyewe:

"Na hatukumpeleka Mtume yeyote isipokuwa kwa lugha ya watu wake iii apate kuwabainishia. Kisha, Mwenyezi Mungu anamuacha kupotea amtakaye (kwa kuwa hataki kufuata ujumbe uliomfikia wazi wazi) na humuongoza amtakaye. Naye ni Mwenye nguvu na Mwenye Hekdma." (14:4)
Aya hii inatufahamisha kuwa kila Mtume alishushiwa Wahyi kwa lugha ya watu wake ili yeye mwenyewe apate kuwabainishia vizuri na wao wapate kumuelewa vizuri. Kwa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa Mwarabu wa kabila Ia Kiquraishi na kwa kuwa Maquraish na Waarabu kwa ujumla ndio watu wake wa mwanzo kuwalingania Uislamu ili wamsaidie kuufikisha ulimwengu mzima. Qur-an ilibidi ishushwe kwa lugha ya Kiarabu cha Kiquraish kilichokuwa fasaha kuliko vilugha vyote vya Kiarabu. Watu wake wasingemuelewa kabisa kama Mtume (s.a.w) angewalignania kwa lugha isiyokuwa ya Kiarabu:

"Na lau kama tungalifanya Qur-an lugha isiyo ya Kiarabu wangelisema: Kwa nini aya zake hazikupambanuliwa? Lo! Lugha isiyokuwa ya Kiarabu na (Mtume) Mwarabu! (Mambo gani hayo)?           " (41:44).

"Na lau tungaliiteremsha juu ya mmoja wa wasiokuwa Waarabu, na akawasomea (kwa ufasaha) wasingalikuwa wenye kuamini." (2 6:198-199)

                              Kutokana na aya hizi tunajifunza kuwa:
(i)        Ni desturi ya Allah (s.w) kumtuma mjumbe wake kwa lugha ya watu wake anaowafikishia.

(ii)       Qur-an imeteremshwa kwa lugha ya Kiarabu kwa kuwa Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa Mwarabu na wale aliowalingania mara ya kwanza walikuwa ni Waarabu.

(iii)      Waarabu wa mwanzo kulinganiwa Uislamu na Mtume (s.a.w) wasingeliukubali ujumbe kama Mtume asingelikuwa Mwarabu na kama angelingania kwa lugha nyingine isiyokuwa ya Kiarabu.

(iv)      Kama Mtume (s.a.w) angelingania kwa lugha nyingine isiyokuwa Kiarabu, ujumbe wake usingelifahamika na watu wake wasingelazimika kuufuata kwa kuwa hawauelewi.

Ujumbe wa Qur-an Utawafikiaje Wale wasio Waarabu au wale Wasiojua Kiarabu?
Si jambo zuri na Si hekima mtu kufikisha ujumbe kwa Kiarabu wakati waSikilizaji wake hawafahamu lugha hiyo. Ni kweli kuwa Kiarabu ni lugha ya Qur-an na lugha aliyoitumia Mtume (s.a.w) kufundishia yale aliyoteremshiwa kutoka kwa Allah (s.w). Hivyo ni lugha ambayo inampasa kila Muislamu ajitahidi kujifunza. Pamoja na umuhimu wa kuifahamu lugha ya Kiarabu, haina maana kuwa anayekijua Kiarabu ndiye Muislamu na yule asiyekijua ni Muislamu mwenye kasoro.

La muhimu ni kuujua ujumbe wa Qur-an na kuendesha maisha ya kila siku kwa mujibu wa ujumbe huo. Ujumbe wa Qur-an unaweza kumfikia kila Muislamu pasina shaka yoyote kwa lugha yake kwa kusoma tafsiri na sherehe ya Qur-an ambayo kwa Rehema ya Allah (s.w) imetolewa katika lugha mbali mbali na wanachuoni wacha Mungu ambao ni mashuhuri katika uliwengu wa Waislamu.

Tukumbuke kuwa Qur-an imeshushwa kwa ajili ya walimwengu wote ambao Allah (s.w) amewajaalia kuzungumza lugha zinazotofautiana (rejea Qur-an (39:22). Naye Mtume (s.a.w) pia ameletwa kwa ajili ya walimwengu wote. Hivyo ili ujumbe wa Qur-an na Sunnah uwafikie walengwa wote, hauna budi kufasiriwa kwa lugha za walengwa wote. Kazi ambayo kwa Rehema ya Allah (s.w) imeshafanyika. Leo hii hapana udhuru kwa mtu yeyote ulimwenguni wa kutoufahamu ujumbe wa Quran kwa sababu si Mwarabu au hajui Kiarabu

                Haja ya Kujifunza Lugha ya Kiarabu kwa Waislamu:
Ipo haja kubwa kwa Waislamu kujifunza lugha ya Kiarabu kuliko ile haja tunayoitambua ya kujifunza lugha za kigeni na za Kimataifa kama vile Kiingereza, Kifaransa, n.k. Kwa mfano hapa Tanzania tunajifunza lugha ya Kiingereza (English) ili tuweze kufaidika kitaaluma, kiuchumi, na kisiasa n.k. Tukijifunza lugha ya Kiarabu tunafaidika na hayo yote pamoja na ziada ifuatayo:

(i) Tutaufahamu ujumbe wa Qur-an na mafundisho ya Mtume (s.a.w) kwa lugha yake ya asili. Daima tafsiri haikosi upungufu japo kidogo.

(ii)Tutaweza kufahamu maana ya undani ya dua na dhikiri mbali mbali tunazoleta katika ibada maalum kama vile swala ambapo haturuhusiwi kutumia lugha nyingine isiyokuwa Kiarabu. Kufahamu maana ya yote tuyasemayo katika swala hutupelekea kuwa na khushui inayotakikana.


(iii)Lugha ya Kiarabu ni chombo cha kuwaunganisha waislamu wote ulimwenguni ili wadumishe udugu na umoja wao kama wanavyotakiwa wawe. Kama Waislamu wanavyoshikamana katika swala kwa kutumia lugha moja ndivyo wanavyotakiwa waelewane na kushikamana katika ibada zote zinazofanywa kimataifa kama vile Ibada ya Hijja