Jumanne, 17 Oktoba 2017

LISHE KULINGANA NA MAKUNDI YA WATU.

                    LISHE KULINGANA NA MAKUNDI YA WATU.

Kila mtu anatkiwa ale chakula kwa kulingana na mahitaji ya mwili wake. Motto anatakiwa ale vyakula maalumu kwa ajili ya kumuwezesha kukuwa vizuri umbo na kiakili. Halikadhalika mama wajawazito wanatakiwa wale vyakula maalumu kwa ajili ya kuwezesha afya ya mama na motto. Wazee, vijana, wafanyakazi na wagojwa wanatakiwa wale vyakula kulingana na hali zao. Hapa tutakuletea lishe kwa kulingana na makundi ya watu.

watoto wanatakiwa kula  vyakula vya protini kwa wingi ili kuwezesha ukuaji wao wa mwili na tishu. Upungufu wa protini unaweza kumpelekea mtoto awe na ukuaji hafifu. Kwa ukuaji mzuri wa meno na mifupa mtoto anatakiwa apewe vyakula vya madini kama madini ya kashian(calcium) upungufu wa madini haya huenda mtoto akawa na ukuaji mbaya wa mifupa. Madini ya zink ni muhimu pia katika ukuaji wa mtoto.


Vitamini B12 ni muhimu kwa ajili ya kuhakikisha utengenezwaji wa seli nyekundu za ndamu. Pia ijulikane kuwa ukuaji mzuri wa mtoto  unategemea kuwepo na damu ya kutosha mwilini ili kuweza kusafirisha gesi ya oxygeni pamoja na viinilishe(nutrients) ndani ya mwili.

Vitamini ni muhimu sana katika ukuaji wa mtoto. Watoto wapewe vyakula vyenye vitamini C kwa wingi kama machungwa, mapapai. Vitamini hivi vinamuwezesha mtoto kutengeneza kinga ya mwili ili kuweza kupamabana na maradhi.
Watoto pia wanatakiwa wapewe vyakula vya wanga kwa wingi ili waweze kupata nguvu ya kutosha kuweza kufanya shughuli zao kama mazoezi ya kutambaa, kukumbia, kusimama n.k.


Wamama wajawazito na wanaonyonyesha.
Wanaonyonyesha na wajawazito wanahitaji kupata vyakula vyenye viinilishe vya kutosha ili kuwezesha ukuaji wa mtoto tumboni , utengenezwaji wa maziwa na kwa ajili ya afya zao wenyewe.


Vyakula vya protini vinahitajika kwa mkiwango kikubwa ili kuwezesha mwili wa mama kujenga misuli vizuri , tishu katika mwili wake na mwili wa mtoto aliye tumboni. Utengenezwaji wa maziwa , usafirishwaji wa damu na ukuaji wa viungo vya mama na mtoto unahitaji protini. Hivyo wamama hawa wapewe protini kwa wingi.


Vyakila vya folic asid na vitamini B vinahitajika kwa ajili ya kuwezesha kupunguza tatizo la kushindwa kujifunguwa kwa njia ya kawaida. Vyakula vya madini ya kashiam(calcium) ni muhimu kwa ukuwji wa mifupa ya mtoto aliye tumboni na kuimarika mwili wa mama pia. Kwani mjamzito asipopewa madini haya mtoto atatumia madini yaliyomo kwa mama na kumfanya mama awe na mifupa dhaifu katika kipindi hiki.


Madini ya chuma ni muhimu katika utengenezwaji wa damu, halikadhalika mtoto anahitaji madini haya ili ayatumie katika wiki ya kwanza ya kuzaliwa. Madini ya zink ni muhimu katika kuwezesha kujifunguwa.(progression of labour) na ukuaji salama wa mtoto aliyoko tumboni.

Wamama wajawazito wapewe vyakula vyenye kambakamba (dietary fiber}. Hivi vitamuwezesha kutopata tatizo la kukosa choo.


Vijana
Vijana wanatakiwa wale sana vyakula vya kuupa mwili nguvu yaani vyakula vya wanga. Pia wale kwa wingi vyakula vyenye protini na madini ya chumvuchumvu kama kashiam(calcium), chuma na phosphorous. Vijana wa kike wanatakiwa wale zaidi vyakula vyenye madini ya chuma ili waweze kuwa na damu ya kutosha hususan wakati wa vipindi vyao.


Wazee
Wazee hawahitaji kuwewa vyakula vya kutia nguvu kwa wingi. Wapewe vyakula vyenye kambakamba ili kuwapunguzia tatizo la kukosa choo na kuwezesha mmeng’enyo wa chakula.


Wazee wapewe vyakula vyenye madini ya chuma, zink na kashiam(calcium) ili kupunguza uwezo wa kupata tatizo la anaemia. Pia madini ya zink ni muhimu katika kuufanya mwili uweze kujenga kinga ya mwili (immune system) na kusaidia kupona kwa urahisi na haraka kwa majeraha.

Ili kupunguza tatizo la kuchoka kwa mifupa (mifupa kuwa dhaifu) kwa wazee wanatakiwa wapewe vyakula vyenye vitamini D na madini ya kahiam(calcium) kwa wingi.

Pia wazee wapewe vyakula ambavyo ni rahisi kutafuna na kumeza. Hii ni kwa sababu wazee wao huwa meno na mifupa yao ni midhaifu pia wana upungufu wa uzalishaji wa mate midomoni mwao kwa mfano baada ya kuwapa nyama wapewe maini.

Wagonjwa.
Wagonjwa wapewe vyakula vyenye viinilishe vyote ili kuwezesha miili yao kuwa na uwezo mkubwa wa kupambana na maradhi.

Matunda na mboga za majani ni muhimu kwa wagonjwa iliwaweze kupata madini na vitamini muhimu kwa ajili ya miili yao. Wagonjwa pia wapewe maji ya kutosha ili kuwezesha miili yao kufanya kazi vizuri.


Matunda yatamuwezesha pia kupambana na maradhi au kupunguza uwezekano wa kuendelea kuuguwa. Wagojwa wapate muda wa kutosha kwa ajili ya kulala na wafanye mazoezi kulingana na hali zao.