Sala
ya Ijumaa
Imeitwa
Sala ya Ijumaa kwa vile inasaliwa siku ya Ijumaa, au kwa yale ya kheri yaliomo
kwenye siku hii. Sala ya Ijumaa ni bora yao ya Sala na siku ya Ijumaa ni bora
yao ya siku. Hivi ni kwa qauli ya Mtume s.a.w.:
"Bora
ya siku zilizochomoza jua juu yake ni siku ya Ijumaa, siku hio ameumbwa Adam
a.s., na siku hio ametiwa Peponi, na siku hio ametoka Peponi, wala hakitasimama
Qiyama isipokuwa siku ya Ijumaa". (Imehadithiwa na Muslim na Abu Daud na
Al Nissaai na Al Tirmidhy).
Sala
ya Ijumaa ni waajibu kwa Qauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, qauli ya Mtume s.a.w.
na itifaqi ya wanazuoni. Ametwambia Mwenyezi Mungu Mtukufu:
"Enyi
mlio amini! Ikiadhiniwa Sala siku ya Ijumaa, nendeni upesi kwenye dhikri ya
Mwenyezi Mungu, na wacheni biashara ……". (Al Jumu'a : 9).
Na
amesema Mtume s.a.w.: