Jumamosi, 17 Februari 2018

UZAZI WA MPANGO KATIKA UISLAMU

                             Kupanga Uzazi katika Uislamu
Kama  ilivyo  haramishwa  kwa  jamii,  Uislamu  umeharamisha  pia
kudhibiti  uzazi  kwa  mtu  binafsi  kwa  khofu  ya  kushindwa  kuwalisha  au
visingizio vingine.  Hata hivyo Uislamu haujawataka watu wazae kiholela.
Kwanza  umekataza  watu  kuzaana  nje  ya  ndoa.    Pili,  walioona
wanatakiwa  wazingatie  umri  baina  ya  mtoto  na  mtoto  mwingine. Kwa
anayetaka kukamilisha muda wa kunyonyesha, basi amnyonyeshe mtoto
wake kwa miaka mwili kama Allah anavyotuambia

Na wanawake waliozaa wawanyonyeshe watoto wao miaka miwili
kamili, kwa anayetaka kukamilisha kunyonyesha…”  (2:233)


Kunyonyesha humsababisha mama mzazi kuchukua muda mkubwa
kabla  ya  kuingia  tena  katika  siku  zake.  Iwapo  mwanamke  atapata  siku
zake  wakati  mtoto  yungali  mchanga  (hajafikia  umri  wa  miaka  miwili),
anatakiwa  ajizuie  asipate  mimba;  kwani  katika  Hadith  iliyosimuliwa  na
Imamu  Muslim,  Mtume  (s.a.w)  amesema  kuwa  mwanamke  akipata
mimba wakati yungali na mtoto mchanga, afya ya mtoto hudhurika.  

Njia za  kuzuia  mimba  katika  kipindi  hiki  cha  kunyonyesha  ni  zile  ambazo
hazina  madhara  ya  kiafya  kwa  baba  wala  mama.    Katika  Hadith
iliyopokelewa na Bukhari na Muslim, Jabir (r.a) amesema kuwa wakati wa
Mtume (s.a.w) wao walikuwa wanatumia njia ya kuzuia mimba inayoitwa
‘azal” (with drawal au coitus interuptus), yaani njia ya kumwaga mbegu za
uzazi nje lakini Mtume (s.a.w) hakuikataza.

Hapa  ifahamike  kwamba  suala  la  kupanga  juu  ya  muda  wa
kunyonya mtoto linamhusu baba na mama na si suala la kuwekewa sera
na taifa; kwani hali za watu zinatafautiana.

Ama kwa mama atakayekuwa na matatizo ya kiafya, ikathibiti kuwa
akibeba  mimba  atadhurika  au  kuhatarisha  maisha  yake,  anaruhusiwa
kufunga kizazi hata kutoa mimba ambayo imeshatunga
>>> Kupata update zetu fuata link zifuatazo.<<<
>>> Bofya hapa kupata yanayojiri katika blog hii UKIWA NA APP YETU

>>> Bofya hapa kuungana nasi youtube ili upate video zetu nyingine

>>> Bofya hapa kupata masomo zaidi ya afya ukiwa na app yetu

>>> Ungana nami kwenye FACEBOOK