Jumapili, 2 Aprili 2017

WALI WA CHOOKO



WALI WA CHOOKO



Mchele kilo1

Chooko ½ kilo

Samli kiasi

Nazi 2 nzuri

Vitunguu thomu kiasi

Bizari nzima kiasi

Vitunguu maji kiasi

Hiliki kiasi

Mdalasini kiasi

Chumvi kiasi

Karafuu chembe 2 au 3

1                    Osha mchele pamoja na chooko uweke pembeni.

2                    Kuna nazi uchuje tui kama la wali wa nazi uliweke.

3                    Menya vitunguu maji, uvioshe uvikate uviweke. Menya vitunguu thomu uvitwange pamoja na bizari na hiliki. Osha vijti vya mdalasini na chembe za karafuu uziweke.


4                    Teleka sufuria utie samli, ikichemka tia vitunguu uvikaange. Baadae tia viungo vyote ulivyovitwanga utie na chembe za karafuu pamoja na vijiti vya mdalasini. Kisha tia tui la nazi. Likianza kufumba tia mchele pamoja na chooko zake utie na chumvi. Acha utokote mpaka wali ukauke. Ukishakauka funika upalie moto.


REFERENCE
click here